HABARI BURUDANI MICHEZO UDAKU AJIRA MUZIKI NA MENGINE MENGI KWENYE UKURASA HUU

  • Breaking News

    Friday, May 18, 2018

    Shambulizi la bunduki lauwa Shuleni Texas



    Watu kadhaa wameuwawa katika shambulizi la kutumia risasi za moto katika shule ya sekondari ya Santa Fe, Texas, imetokea Ijumaa, kwa mujibu wa vyombo vya usalama vya eneo hilo.
    Uongozi wa shule hiyo umesema kuwa kuna majeruhi katika shambulizi hilo, lakini hawajatoa idadi yao.
    Wamiliki wa Shule ya kujitegemea ya Santa Fe (ISD) wametoa tamko kuwa "hali fulani imetokea katika shule hiyo ambapo kulikuwa na mshambuliaji aliyetumia bunduki.
    Tayari uongozi umeweka vizuizi katika eneo hilo.
    Polisi na wahudumu wa masuala ya dharura walipelekwa katika eneo la tukio, pamoja na wawakilishi wa serikali kuu kutoka katika kitengo kinachokabiliana na Ulevi, Tumbaku, Silaha na Mabomu.
    Santa Fe iko katika eneo la kusini mashariki ya Texas kati ya mji wa Houston na Galveston.

    No comments:

    Loading...

    AJIRA

    SIMU

    AFYA

    UDAKU